SYRIA: Nafasi ya Al Assad ya Kusitisha Umwagaji Damu Kwa Wahariri: Taarifa ifuatayo imetolewa na Shirika la Habari la Falme za Kiarabu (WAM)
ABU DHABI, Aprili 5 (WAM) - Uamuzi wa rais wa Syria, Bashar Al Assad wa kukubali mpango wa amani na kuruhusu timu za wanachama wa Umoja wa Mataifa kuingia nchini Syria kunampatia fursa nzuri ya kujaribu na kufufua hali ya kujali kwake haki za binadamu ambayo ilianza kufifia. Kwa maana hiyo, fursa hiyo isipokelewe kwa kuendelea kuenea kwa ghasia kabla ya tarehe ya mwisho ya Aprili 10 iliyopangwa kusitisha vita nchini humo, limetoa maoni gazeti la kila siku katika Muungano wa Falme za Kiarabu (UAE).
Mapendekezo yaliyotolea na Kofi Annan yanatoa wito wa kuondolewa kwa vikosi vya kijeshi na vifaa vizito vya kivita katika maeneo yenye wakazi wengi – kwanza na serikali ya Syria halafu vikifuatiwa na vikosi vya upinzani. "Kusitisha mapigano kunatarajiwa kujenga mazingira ya mazungumzo yenye lengo la kufikia ufumbuzi wa kisiasa," lilisema gazeti la kila siku la Gulf News katika tahariri yake.
Vikosi vya Syria vimekubali kuzungumza ambapo siku za nyuma havikuweza kukubali ila kuamua kutumia njia ya ghasia kutokana na kudai kuwa waasi ndiyo wa kwanza kuwachokoza. Ni mbinu inayofaa kuungwa mkono na inaelezea ni kwa nini jeshi linachukua hatamu katika viunga vya jiji vyenye wakazi wengi. "Ukweli kwamba upinzani umekuwa dhaifu, umegawanyika, wamekuwa wakipigana wenyewe kwa wenyewe na kugombea madaraka kulimsaidia rais Al Assad kukubali mpango huu.
"Wakati hataki kupoteza udhibiti, Al Assad lazima kufanya jitihada za kweli kuvuna matunda ya mchakato wa kidiplomasia ambao kwa sasa ni lazima kuukubali," liliongeza gazeti hilo. (WAM)
(END/2012)
|
|
|