UAE: Yasaini Makubaliano na Ureno Juu ya Ushirikiano katika Nishati Mbadala, Elimu ya Juu Kwa Wahariri: Taarifa ifuatayo imetolewa na Shirika la Habari la Falme za Kiarabu (WAM)
LISBON, Aprili 28 (WAM) - Waziri wa Mambo ya Nje wa Muungano wa Falme za Kiarabu (UAE) Sheikh Abdullah bin Zayed Al Nahyan alikutana jana na mwenzake wa Ureno Paulo Portas na kujadili mahusiano baina ya nchi hizo mbili na jinsi ya kuongeza ushirikiano katika nyanja zote.
Sheikh Abdullah na Portas walisaini aina mbili za makubaliano ya kushirikiana kwa nchi hizo mbili katika nyanja ya sekta ya nishati mbadala na elimu ya juu na utafiti wa kisayansi.
Mkutano wao ulihudhuriwa pia na Sheikh Abdullah Mohammed Al Hamed, Mkurugenzi wa Masuala ya Ulaya katika Wizara ya Mambo ya Kigeni, Mohammed Mahmoud Al Khawaja, Mshauri katika wizara hiyo, Saleh Al Suwaidi, Msaidizi wa Waziri wa Mambo ya Nje anayeshughulikia Masuala ya Uchumi, na Saqr Nasser Ahmed Al Raisi, Balozi wa UAE nchini Ureno.
(END/2012)
|
|
|